Linda afya ya Moyo kwa kufanya hivi 00014
Miongoni mwa magonjwa ambayo husumbua watu wengi kwa kiwango kikubwa ni moyo, hivyo ili kuweza kulinda afya ya moyo wako ili usipate magonjwa hayo ya moyo unatakiwa kufanya yafuatayo;


  1. Pima shinikizo la damu angalau mara moja kwa mwaka.
  2. Hakikisha unakuwa na uzito  sahihi.
  3. Fanya mazoezi walau nusu saa kwa siku.
  4. Punguza matumizi ya chumvi  kwenye chakula. Hapa tunanzungumzia chumvi ya mezani ambayo huongezwa kwenye vyakula kama vile nyama choma, chipsi n.k
  5. Kila wakati hakikisha unakula zaidi  matunda,mboga za majani na vyakula ambavyo havina  mafuta.
  6. Punguza matumizi na unjwaji wa pombe.
  7. Iwapo umegundulika kuwa na tatizo la shinikizo la damu,tumia dawa kama ulivyoelekezwa na watalamubwa afya na si vinginevyo.